Ezekiel 30:13-18
13 a“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “ ‘Nitaangamiza sanamuna kukomesha vinyago katika Memfisi ▼
▼ Kiebrania ni Nofu.
Hapatakuwepo tena na mkuu katika nchi ya Misri,
nami nitaeneza hofu katika nchi nzima.
14 cNitaifanya Pathrosi ▼
▼ Pathrosi ni Misri ya Juu.
kuwa ukiwana kuitia moto Soani,
nami nitaipiga kwa adhabu Thebesi ▼
▼ Thebesi kwa Kiebrania ni No (au No-Amoni), mji katika Misri.
15 Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu, ▼
▼ Kiebrania ni Sini.
ngome ya Misri,
nami nitakatilia mbali
makundi ya wajeuri wa Thebesi.
16 gNitaitia moto nchi ya Misri;
Pelusiumu itagaagaa kwa maumivu makuu.
Thebesi itachukuliwa na tufani,
Memfisi itakuwa katika taabu daima.
17 hWanaume vijana wa Oni ▼
▼ Yaani Heliopoli (Mji wa Jua).
na wa Pi-Besethi ▼▼ Yaani Bubasti.
wataanguka kwa upanga
nayo hiyo miji itatekwa.
18 kHuko Tahpanhesi mchana utatiwa giza
nitakapovunja kongwa la Misri;
hapo kiburi cha nguvu zake kitakoma.
Atafunikwa na mawingu
na vijiji vyake vitatekwa.
Copyright information for
SwhKC